Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 24:2 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

maana fikira zao zote ni juu ya ukatili, hamna jema lolote litokalo midomoni mwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

maana fikira zao zote ni juu ya ukatili, hamna jema lolote litokalo midomoni mwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

maana fikira zao zote ni juu ya ukatili, hamna jema lolote litokalo midomoni mwao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema kuhusu kuleta madhara.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 24:2
21 Marejeleo ya Msalaba  

Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Na mioyo yao hutunga udanganyifu.


Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,


Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huchochea vita.


Usinikokote pamoja na wasio haki, Wala pamoja na watenda maovu. Wawaambiao jirani zao maneno ya amani, Lakini mioyoni mwao mna madhara.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usikubali.


Mtu afikiriye kutenda maovu, Watu watamwita mtundu;


Mna upotovu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.


Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;


Basi kwa ajili ya hayo Mtakatifu wa Israeli asema hivi, Kwa sababu mwalidharau neno hili, na kutumainia jeuri na ukaidi, na kuyategemea hayo;


Hakuna anayeshitaki kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.


Bali macho yako na moyo wako hauna utakalo ila kutamani, na kumwaga damu isiyo na hatia, na kudhulumu, na kutenda jeuri.


Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.


akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyooka?


Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera.