Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 22:4 - Swahili Revised Union Version

Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ukinyenyekea na kumcha Mwenyezi-Mungu, utapata tuzo: Fanaka, heshima na uhai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ukinyenyekea na kumcha Mwenyezi-Mungu, utapata tuzo: Fanaka, heshima na uhai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ukinyenyekea na kumcha Mwenyezi-Mungu, utapata tuzo: fanaka, heshima na uhai.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Unyenyekevu na kumcha Mwenyezi Mungu huleta utajiri, heshima na uzima.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Unyenyekevu na kumcha bwana huleta utajiri, heshima na uzima.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 22:4
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kumcha BWANA huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.


Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.


Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima.


Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.


Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu; Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kulia, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.


Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye BWANA, ndiye atakayesifiwa.


Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha BWANA ni hazina yake ya akiba.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Basi wakati huo huo fahamu zangu zikanirudia, na kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu, enzi yangu na fahari yangu zikanirudia; na mawaziri wangu, na madiwani wangu, wakaja kunitafuta; nami nikathibitika katika ufalme wangu, nikaongezewa enzi kupita kiasi.


Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.


Maana, mazoezi ya viungo vya mwili yana manufaa kidogo, lakini utauwa una manufaa ya kila aina; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.


Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.