Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 16:1 - Swahili Revised Union Version

Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Binadamu hupanga mipango yake, lakini kauli ya mwisho ni yake Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Binadamu hupanga mipango yake, lakini kauli ya mwisho ni yake Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Binadamu hupanga mipango yake, lakini kauli ya mwisho ni yake Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu, bali jibu la ulimi hutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu, bali jibu la ulimi hutoka kwa bwana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 16:1
24 Marejeleo ya Msalaba  

Nenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, BWANA asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?


Ikawa makamanda wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Mfalme wa Israeli ni huyu. Basi wakamgeukia ili wapigane naye; lakini Yehoshafati akalia, na BWANA akamsaidia; Mungu akawaondoa kwake.


Na ahimidiwe BWANA, Mungu wa baba zetu, aliyetia neno kama hilo katika moyo wa mfalme, kuipamba nyumba ya BWANA iliyoko Yerusalemu.


Ee Bwana, nakusihi, litege sikio lako, uyasikilize maombi ya mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako, wanaofurahi kulicha jina lako; nakuomba sana; unifanikishe mimi, mtumishi wako, leo, ukanijalie rehema mbele ya mtu huyu. (Maana, nilikuwa mnyweshaji wa mfalme).


Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.


BWANA, utayasikia matakwa ya wanyonge, Uutaidhibiti mioyo yao, utalitega sikio lako.


Unielekeze moyo wangu katika shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.


Nawe utasema naye, na kuyatia maneno kinywani mwake; nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na pamoja na kinywa chake, na kuwafundisheni mtakayofanya.


Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.


Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la BWANA ndilo litakalosimama.


Mwenendo wa mtu watoka kwa BWANA; Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?


Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; Kama mifereji ya maji huugeuza popote apendapo.


Ee BWANA, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.


Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo wa Tito.


Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.