Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 12:17 - Swahili Revised Union Version

Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli, lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli, lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli, lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 12:17
15 Marejeleo ya Msalaba  

Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.


Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.


Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu; Bali atoaye uongo hudanganya.


Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.


Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.


Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.


Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako.


Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.


Haya ndiyo mtakayoyatenda; kila mtu na aseme ukweli na jirani yake; katika malango yenu toeni hukumu za kweli na ziletazo amani;


Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wizi, ushuhuda wa uongo, na matukano;


Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;


Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati;


Nanyi muwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo.