Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 24:28 - Swahili Revised Union Version

28 Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

28 Usishuhudie bure dhidi ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

28 Usishuhudie bure dhidi ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

28 Usishuhudie bure dhidi ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

28 Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako.

Tazama sura Nakili




Methali 24:28
24 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ijapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.


Mashahidi wa udhalimu wanasimama, Wananiuliza mambo nisiyoyajua.


Maana bila sababu wamenifichia wavu, Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu.


Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.


Usimshuhudie jirani yako uongo.


Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.


Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.


Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.


Mtu amshuhudiaye jirani yake uongo Ni nyundo, na upanga, na mshale mkali.


Ndivyo alivyo amdanganyaye mwenzake, Na kusema, Je! Sikufanya mzaha tu?


Msiibe, wala msidanganye, wala msiambiane uongo.


Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya BWANA, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la mapatano, au la kunyang'anya, au kumwonea mwenziwe;


au kupata kitu kilichopotea na kutenda la uongo juu yake, na kuapa kwa uongo; katika mambo hayo yote mojawapo atakalolitenda mtu, na kufanya dhambi kwalo;


Akasema, Kwa nini? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulubiwe.


Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.


Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake.


Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;


Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.


Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo