Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 1:8 - Swahili Revised Union Version

Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyapuuze mafundisho ya mama yako;

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyapuuze mafundisho ya mama yako;

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyapuuze mafundisho ya mama yako;

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 1:8
20 Marejeleo ya Msalaba  

Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usikubali.


Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.


Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;


Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.


Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.


Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.


Maneno ya mfalme Lemueli; mausia aliyofundishwa na mama yake.


Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu, Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!


Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako.


Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.


Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;


Kila mtu na amche mama yake, na baba yake, nanyi mtazitunza Sabato zangu; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, akiwa amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.


Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.


nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika nyanya yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo.


Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza.


Mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu BWANA amekusudia kuwaua.