Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Samueli 23:6 - Swahili Revised Union Version

Lakini hatawachipuza watu wasiofaa; Watakuwa wote kama miiba ya nyikani ya kutupwa, Maana haichukuliki kwa mkono,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini wasiomcha Mungu wote ni kama miiba inayotupwa tu, maana haiwezi kuchukuliwa kwa mkono;

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini wasiomcha Mungu wote ni kama miiba inayotupwa tu, maana haiwezi kuchukuliwa kwa mkono;

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini wasiomcha Mungu wote ni kama miiba inayotupwa tu, maana haiwezi kuchukuliwa kwa mkono;

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini hatawachipuza watu wasiofaa; Watakuwa wote kama miiba ya nyikani ya kutupwa, Maana haichukuliki kwa mkono,

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Samueli 23:6
12 Marejeleo ya Msalaba  

michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;


Basi ilitukia ya kwamba kulikuwapo mtu asiyefaa, jina lake akiitwa Sheba, mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga tarumbeta, akasema, Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni kila mtu hemani kwake, enyi Israeli.


Kama fahirisi kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti.


Mimi sina hasira ndani yangu; Kama mbigili na miiba ingekuwa mbele zangu, Ningepanga vita juu yake, Ningeiteketeza yote pamoja.


Nao mataifa watakuwa kama kuchoma chokaa, kama miiba iliyokatika, iteketezwayo motoni.


Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma inakuzunguka, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.


Mtu aliye mwema miongoni mwao ni kama mbigili; mtu aliye mwenye adili miongoni mwao ni mbaya kuliko boma la michongoma; hiyo siku ya walinzi wako, yaani, siku ya kujiliwa kwako, imefika; sasa kutatokea kufadhaika kwao.


Kwa maana kama miiba wametatana, kama walevi wamelewa, watateketezwa kama mabua makavu.


Mwana wa Adamu atawatuma malaika wake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,


Kumetoka katikati yako mabaradhuli kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;


Basi, hao wana wa Eli walikuwa watu wasiofaa kitu; hawakumjali BWANA,


Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.