Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mwanzo 3:18 - Swahili Revised Union Version

18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Ardhi itakuzalia michongoma na magugu, nawe itakubidi kula majani ya shambani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Ardhi itakuzalia michongoma na magugu, nawe itakubidi kula majani ya shambani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Ardhi itakuzalia michongoma na magugu, nawe itakubidi kula majani ya shambani.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Itakuzalia miiba na mibaruti, nawe utakula mimea ya shambani.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;

Tazama sura Nakili




Mwanzo 3:18
20 Marejeleo ya Msalaba  

Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nilikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;


kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.


akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nikiwa uchi, nami nitarudi tena huko uchi vile vile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.


Miiba na imee badala ya ngano, Na magugu badala ya shayiri. Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.


Mavuno yake wale wenye njaa huyala, Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani, Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.


Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;


Wamrudisha mtu mavumbini, usemapo, Rudini, enyi wanadamu.


Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu; Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.


Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.


Juu ya nchi ya watu wangu itamea michongoma na mibigili; naam, juu ya nyumba za furaha katika mji ulio na shangwe;


nami nitaliharibu; wala halitapogolewa wala kulimwa, bali litamea mbigili na miiba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Tena itakuwa katika siku hiyo kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja, iliyopata fedha elfu moja, patakuwa mahali pa mbigili na miiba tu.


Mtu atakayekwenda huko atakwenda na mishale na upinde; kwa sababu nchi yote itakuwa ina mbigili na miiba.


Wamepanda ngano, lakini watavuna miiba; wamejiumiza nafsi zao, lakini hawatakuwa na faida; naam, tahayarini kwa ajili ya matunda yenu, kwa sababu ya hasira kali ya BWANA.


Maana BWANA awaambia hivi watu wa Yuda na Yerusalemu Ulimeni udongo katika konde zenu, wala msipande mbegu kati ya miiba.


Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga;


Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.


bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.


jueni hakika ya kuwa BWANA, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hadi mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo BWANA, Mungu wenu, amewapa ninyi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo