Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mika 7:7 - Swahili Revised Union Version

Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini mimi namtumainia Mwenyezi-Mungu, namtazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini mimi namtumainia Mwenyezi-Mungu, namtazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini mimi namtumainia Mwenyezi-Mungu, namtazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini mimi, namtazama Mwenyezi Mungu kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini mimi, namtazama bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mika 7:7
33 Marejeleo ya Msalaba  

Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.


Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa niliwaombea.


Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja, Na neno lake nimelitumainia.


Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.


Utulie mbele za BWANA, Nawe umngojee kwa subira; Usihangaike juu ya afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu apangaye maovu.


Kwa kuwa nakungoja Wewe, BWANA, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.


Uniite siku ya mateso; Nitakuokoa, nawe utanitukuza.


Wewe usikiaye maombi, Wote wenye mwili watakujia.


Je! Utatufanyia hasira hata milele? Utadumisha ghadhabu kizazi hadi kizazi?


Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.


Katika siku hiyo mwanadamu atamwangalia Muumba wake, na macho yake yatamtazama Mtakatifu wa Israeli.


Katika siku hiyo watasema, Tazama, huyu ndiye Mungu wetu, Ndiye tuliyemngoja atusaidie; Huyu ndiye BWANA tuliyemngoja, Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake.


Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.


Nami nitamngojea BWANA, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia.


BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.


Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuri liwakalo moto; naye atatuokoa mkononi mwako, Ee mfalme.


Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.


Ee BWANA, nakulilia wewe; Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani, Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.


Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu kuhusu kulalamika kwangu.


Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.


Na kama mwanamke hakuwa na unajisi lakini yu safi; ndipo ataachiliwa, naye atazaa wana.