Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 25:6 - Swahili Revised Union Version

Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme; Wala usisimame mahali pa watu wakuu;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Usijipendekeze kwa mfalme, wala usijifanye mtu mkubwa,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Usijipendekeze kwa mfalme, wala usijifanye mtu mkubwa,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Usijipendekeze kwa mfalme, wala usijifanye mtu mkubwa,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme; Wala usisimame mahali pa watu wakuu;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 25:6
15 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.


Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?


Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini, Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.


Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.


Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme, Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki.


Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele; Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu. Yale uliyoyaona kwa macho,


Mwingine na akusifu wala si kinywa chako mwenyewe; Mtu mgeni wala si midomo yako wewe.


Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.


Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe,


Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha makabila ya Israeli? Naye BWANA akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.