Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 16:27 - Swahili Revised Union Version

Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara; Katika midomo yake mna moto uteketezao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu mwovu hupanga uovu; maneno yake ni kama moto mkali.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu mwovu hupanga uovu; maneno yake ni kama moto mkali.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu mwovu hupanga uovu; maneno yake ni kama moto mkali.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya, maneno yake ni kama moto uunguzao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya, maneno yake ni kama moto uunguzao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara; Katika midomo yake mna moto uteketezao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 16:27
15 Marejeleo ya Msalaba  

Basi ilitukia ya kwamba kulikuwapo mtu asiyefaa, jina lake akiitwa Sheba, mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga tarumbeta, akasema, Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni kila mtu hemani kwake, enyi Israeli.


Nafsi yangu i kati ya simba, Nitastarehe kati yao waliowaka moto. Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, Na ndimi zao ni upanga mkali.


Nafsi yake mfanyakazi hujifanyia kazi; Maana kinywa chake humtia bidii.


Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.


Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.


Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.


Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;


Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotovu.


Mna upotovu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.


Ole wao wavutao uovu kwa kamba za ubatili, na dhambi kama kwa kamba za gari!


Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa BWANA wa majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya ubatili?


Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfululizo wa maumbile, nao huwashwa moto na Jehanamu.


Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.