Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 6:12 - Swahili Revised Union Version

12 Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotovu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu, huzururazurura akisema maneno mapotovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu, huzururazurura akisema maneno mapotovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu, huzururazurura akisema maneno mapotovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

12 Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotovu.

Tazama sura Nakili




Methali 6:12
26 Marejeleo ya Msalaba  

Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.


Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,


Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.


Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.


Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye?


Midomo ya mwenye haki huyajua yatakayokubaliwa; Bali kinywa chao wasio haki hunena ukaidi.


Haki yao wenye haki itawaokoa; Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.


Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara; Katika midomo yake mna moto uteketezao.


Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.


Mtenda mabaya husikiliza midomo ya uovu; Na mwongo hutega sikio lake kusikiliza ulimi wa madhara.


Ili kukuokoa na njia ya uovu, Na watu wanenao yaliyopotoka;


Maana mtu mjeuri ni chukizo kwa BWANA, Bali siri yake ni pamoja na wanyofu.


Jiepushe na kinywa cha ujeuri, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.


Mna upotovu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.


Kumcha BWANA ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.


Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama tini zilizotangulia kuiva; na kikapu cha pili kilikuwa na tini mbovu sana zisizoweza kuliwa, kwa kuwa zilikuwa mbovu sana.


Enyi wazawa wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.


tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawafuatie wao.


Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.


Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu.


Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfululizo wa maumbile, nao huwashwa moto na Jehanamu.


Naye Eliabu, mkubwa wake, alisikia hapo alipoongea na watu; na hasira yake Eliabu ikawaka juu ya Daudi, akasema, Mbona wewe umeshuka hapa? Na kondoo wale wachache umemwachia nani kule nyikani? Mimi nakujua kiburi chako, na ubaya wa moyo wako; maana umeshuka ili upate kuvitazama vita.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo