Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 13:9 - Swahili Revised Union Version

Nuru ya mwenye haki yang'aa sana; Bali taa ya mtu mbaya itazimika.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwadilifu hungaa kama taa iwakayo vizuri, lakini waovu ni kama taa inayozimika.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwadilifu hungaa kama taa iwakayo vizuri, lakini waovu ni kama taa inayozimika.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwadilifu hung'aa kama taa iwakayo vizuri, lakini waovu ni kama taa inayozimika.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nuru ya mwenye haki hung’aa sana, bali taa ya mwovu itazimwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nuru ya mwenye haki hung’aa sana, bali taa ya mwovu itazimwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nuru ya mwenye haki yang'aa sana; Bali taa ya mtu mbaya itazimika.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 13:9
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili Daudi, mtumishi wangu, apate kuwa na taa siku zote mbele zangu katika Yerusalemu, mji ule niliouchagua niweke jina langu huko.


Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimwa? Na msiba wao kuwajia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?


Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani, Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;


Nuru huwaangaza wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki.


Nuru humwangazia mwenye haki, Na furaha ni kwa wanyofu wa moyo.


Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.


Fidia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lolote.


Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.


Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu; Taa ya mtu mbaya itazimika.


Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu.


Nami nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu, na kuzifanya nyota zake kuwa giza; nami nitalifunika jua kwa wingu, wala mwezi hautatoa nuru yake.


Kwa nini basi jina la baba yetu kufutwa katika jamaa zake kwa sababu alikuwa hana mwana wa kiume? Tupe sisi urithi pamoja na ndugu zake baba yetu.


Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.