Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 12:28 - Swahili Revised Union Version

Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Uadilifu ni njia ya uhai, lakini uovu huongoza katika mauti.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Uadilifu ni njia ya uhai, lakini uovu huongoza katika mauti.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Uadilifu ni njia ya uhai, lakini uovu huongoza katika mauti.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 12:28
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima; Mazao ya wabaya huielekea dhambi.


Hazina za uovu hazifaidii kitu; Bali haki huokoa na mauti.


Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.


Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa BWANA.


Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa; Na miaka ya maisha yako itaongezwa.


Nawe waambie watu hawa, BWANA asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.


tena ikiwa amezifuata sheria zangu, na kuzishika hukumu zangu; mtu huyu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana MUNGU.


ili kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala katika mauti, vivyo hivyo kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.


Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;


Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;


akawaambia, Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo nashuhudia kwenu hivi leo; nayo waamuruni watoto wenu, wayatunze na kuyafanya maneno yote ya torati hii.


Kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa na yeye.


Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki;


Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.