Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 8:18 - Swahili Revised Union Version

Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng'ambo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ngambo ya ziwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ngambo ya ziwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa alipoona makundi mengi yamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake wavuke hadi ng’ambo ya ziwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa alipoona makutano mengi wamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake wavuke mpaka ng’ambo ya ziwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng'ambo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 8:18
10 Marejeleo ya Msalaba  

Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande katika mashua na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.


Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.


Siku hiyo kulipokuwa jioni, Yesu akawaambia, Na tuvuke mpaka ng'ambo.


Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng'ambo katika ile mashua, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.


Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande mashuani, watangulie kwenda ng'ambo hata Bethsaida, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.


Akawaacha, akapanda tena katika mashua, akaenda zake hadi ng'ambo.


Ikawa siku zile mojawapo alipanda katika mashua yeye na wanafunzi wake, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng'ambo ya ziwa. Wakatweka matanga.


Kisha Yesu, alipotambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye mfalme, akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake.