Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Marko 3:10 - Swahili Revised Union Version

Maana aliponya wengi, hata wote waliokuwa na misiba wakamrukia wapate kumgusa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana aliponya wengi, hata wote waliokuwa na misiba wakamrukia wapate kumgusa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Marko 3:10
18 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini BWANA akampiga Farao na nyumba yake mapigo makuu, kwa ajili ya Sarai, mkewe Abramu.


Kisha hapo hiyo nyama ilipokuwa ikali kati ya meno yao, hawajaitafuna bado, hasira za BWANA ziliwaka juu ya watu, BWANA akawapiga watu kwa pigo kuu mno.


Naye Yesu hali akiyafahamu hayo akaondoka huko; na watu wengi wakamfuata; akawaponya wote,


Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.


nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu; na wote waliogusa wakaponywa kabisa.


Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya kila ugonjwa na maradhi ya kila namna waliyokuwa nayo watu.


Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, nenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena.


Na kila alikokwenda, akiingia vijijini, au mijini, au mashambani, wakawaweka wagonjwa sokoni, wakamsihi waguse angaa pindo la vazi lake; nao wote waliomgusa wakapona.


Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.


Akaingia katika mashua moja, ndiyo yake Simoni, akamtaka aipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano akiwa katika mashua.


Na makutano yote walikuwa wakitaka kumgusa, kwa sababu uweza ulikuwa ukimtoka ukiwaponya wote.


Na mtumwa wake afisa mmoja alikuwa mgonjwa, karibu kufa; naye ni mtu aliyempenda sana.


Na saa ile ile aliwaponya wengi magonjwa yao, na misiba, na pepo wabaya; na vipofu wengi aliwakirimia kuona.


hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya mikeka na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao.


Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humuonya Naye humpiga kila mwana amkubaliye.