Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 1:30 - Swahili Revised Union Version

Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu; umepata kibali kwa Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, umepata kibali kwa Mwenyezi Mungu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 1:30
13 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA.


usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kulia wa haki yangu.


Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema BWANA, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.


BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.


Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo, ni mimi; msiogope.


Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.


Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto wa kiume, na jina lake utamwita Yohana.


Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.


akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.


Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani awezaye kutupinga?


Hata tunathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?