Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Samueli 15:1 - Swahili Revised Union Version

Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Baada ya tukio hilo, Absalomu alijipatia gari, farasi na watu hamsini wa kumtangulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Baada ya tukio hilo, Absalomu alijipatia gari, farasi na watu hamsini wa kumtangulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Baada ya tukio hilo, Absalomu alijipatia gari, farasi na watu hamsini wa kumtangulia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Samueli 15:1
11 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA asema hivi, Angalia, nitakuzushia uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako hadharani.


Naye mfalme akawaambia, Twaeni pamoja nanyi watumishi wa bwana wenu, mkampandishe Sulemani mwanangu juu ya nyumbu wangu mimi mkamteremshe mpaka Gihoni;


Ndipo Adonia mwana wa Hagithi akatakabari, akasema, Mimi nitakuwa mfalme. Akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, na watu hamsini wapige mbio mbele yake.


Hawa wanataja magari na hawa farasi, Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.


Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.


Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.


Apendaye ugomvi hupenda dhambi; Auinuaye sana mlango wake hutafuta uharibifu.


Ila asifanye farasi wake kuwa wengi, wala asiwarudishe watu Misri, ili apate kufanya farasi kuwa wengi; kwa kuwa BWANA amewaambia, Tangu sasa msirudie tena njia ile.


Akasema, Mfalme atakayewatawala ninyi atakuwa na desturi hii; atatwaa wana wenu na kuwaweka kwake, katika magari yake, na kuwa wapanda farasi wake; nao watapiga mbio mbele ya magari yake.