Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Petro 3:10 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme uongo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme uongo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Petro 3:10
24 Marejeleo ya Msalaba  

Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.


Yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni, Na uhai wangu utautazama mwanga.


Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi; Zakimbia, wala hazioni mema.


Ili niuone wema wa wateule wako. Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako, Na kujisifu pamoja na watu wako.


Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA Katika nchi ya walio hai.


Atakwenda kwenye kizazi cha baba zake Hawataona nuru hata milele.


Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu anayeshikamana naye.


Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.


Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote.


Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa BWANA.


Moyoni mwangu nikapeleleza jinsi ya kuuburudisha mwili kwa mvinyo, na (moyo wangu ungali ukiniongoza kwa hekima) jinsi ya kushikana na upumbavu, hata niyaone yaliyo mema ya kuwafaa wanadamu, ili wayafanye hayo chini ya mbingu siku zote za maisha yao.


Akamwambia, Kwa nini uniulize kuhusu wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.


Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.


Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.


Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.


Kwa maana si jambo lisilofaa kwenu; maana, ni maisha yenu, na kwa jambo hili mtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi mwivukiayo Yordani kuimiliki.


Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, ili hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.


Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.


Yeye hakutenda dhambi, wala udanganyifu haukuwapo kinywani mwake.


Na katika vinywa vyao haukuonekana uongo. Maana hawana mawaa.