Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Petro 3:11 - Swahili Revised Union Version

11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Ajiepushe na uovu, atende mema, atafute amani na kuizingatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Ajiepushe na uovu, atende mema, atafute amani na kuizingatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Ajiepushe na uovu, atende mema, atafute amani na kuizingatia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Mtu huyo lazima aache uovu, akatende mema; lazima aitafute amani na kuifuatilia sana.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Mtu huyo lazima aache uovu, akatende mema; lazima aitafute amani na kuifuatilia sana.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.

Tazama sura Nakili




1 Petro 3:11
37 Marejeleo ya Msalaba  

Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ijapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.


Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu.


Ee BWANA, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo.


Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.


Jiepushe na uovu, utende mema, Na kukaa hata milele.


Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu; Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.


Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.


Usiwe na hekima machoni pako; Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.


ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.


Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.


Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]


maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamko nami sikuzote.


Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.


Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.


Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya; kuponya roho au kuangamiza?


Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.


Ikiwezekana, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.


Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.


Basi kama ni hivyo, na mfuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana.


Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na muwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,


Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo.


Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya.


Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,


Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.


Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.


Waamuru watende mema, wawe matajiri katika kutenda mema, wawe wakarimu na wawe tayari kushiriki na wengine;


Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;


Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.


Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.


Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana uko juu ya watenda mabaya.


Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.


Yeftha akatuma wajumbe mara ya pili waende kwa huyo mfalme wa wana wa Amoni;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo