Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yakobo 4:10 - Swahili Revised Union Version

Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Jinyenyekezeni mbele za Mwenyezi Mungu, naye atawainua.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Jinyenyekezeni mbele za Mwenyezi Mungu, naye atawainua.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yakobo 4:10
19 Marejeleo ya Msalaba  

ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekeza, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.


Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.


Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.


Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.


BWANA huwategemeza wenye upole, Huwaangusha chini wenye jeuri.


Na sasa kichwa changu kitainuka Juu ya adui zangu wanaonizunguka. Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake; Nitaimba, naam, nitamhimidi BWANA.


Uwaokoe watu wako, uubariki urithi wako, Uwachunge, uwachukue milele.


Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.


Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Bwana MUNGU asema hivi; Kiondoe kilemba, livue taji; haya hayatakuwa tena kama yalivyo; kikweze kilicho chini, kakishushe kilichoinuka.


Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.


Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewainua.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;


BWANA hufukarisha mtu, na hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu.


Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake; Bali waovu watanyamazishwa gizani, Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;