Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 9:4 - Swahili Revised Union Version

Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini msile nyama yenye damu, kwani uhai uko katika damu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini msile nyama yenye damu, kwani uhai uko katika damu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini msile nyama yenye damu, kwani uhai uko katika damu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu, kwa maana damu ni uhai.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 9:4
15 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Mnakula nyama pamoja na damu yake, na kuviinulia vinyago vyenu macho yenu, na kumwaga damu; je, mtaimiliki nchi hii?


Msile kitu chochote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi.


Neno hili litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa.


Tena msiile damu yoyote, ama ya ndege, ama ya mnyama, katika nyumba zenu zote.


bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.


sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,


yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu.


Lakini msiile damu; imwageni juu ya nchi kama maji.


Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama.


Msile nyamafu yoyote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye.


Pamoja na haya usile damu yake; uimwage nchi kama maji.


Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;


Basi watu wakazirukia zile nyara, wakatwaa kondoo, na ng'ombe, na ndama, na kuwachinja papo hapo juu ya nchi, nao wale watu walikuwa wakiwala pamoja na damu.