Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 6:8 - Swahili Revised Union Version

Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini Noa alipata fadhili mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini Noa alipata fadhili mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini Noa alipata fadhili mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini Nuhu akapata kibali machoni pa Mwenyezi Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini Nuhu akapata kibali machoni pa bwana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 6:8
23 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, mtumwa wako ameona kibali machoni pako, nawe umezidisha rehema zako ulizonifanyia kwa kuponya nafsi yangu, nami siwezi kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa.


BWANA huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.


Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.


Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa BWANA.


BWANA asema hivi, Watu wale walioachwa na upanga walipata neema jangwani; yaani, Israeli, hapo nilipokwenda kumstarehesha.


wajapokuwa watu hawa watatu, Nuhu, na Danieli, na Ayubu, kuwamo ndani yake, wangejiokoa nafsi zao wenyewe tu kwa haki yao, asema Bwana MUNGU.


Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.


Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.


Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.


aliyepata fadhili mbele za Mungu, naye aliomba ampatie Mungu wa Yakobo maskani.


Lakini ikiwa ni kwa neema, haiwi kwa matendo tena, au hapo neema isingekuwa neema.


Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nilizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.


Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake,


Bwana na amjalie ili kwamba apate rehema machoni pa Bwana siku ile. Na jinsi alivyonihudumia kwa mengi huko Efeso, wewe unajua sana.


Maana neema ya Mungu iwaokoao wanadamu wote imefunuliwa;


ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu.


Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.


watu wasiotii hapo zamani, wakati Mungu alipowavumilia kwa subira, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.


wala hakuuachilia ulimwengu wa kale, bali alimhifadhi Nuhu, mjumbe wa haki, na watu wengine saba, hapo alipoleta Gharika juu ya ulimwengu wa wasiomcha Mungu;