Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 11:7 - Swahili Revised Union Version

Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Haya, na tushuke chini na kuivuruga lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Haya, na tushuke chini na kuivuruga lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Haya, na tushuke chini na kuivuruga lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 11:7
20 Marejeleo ya Msalaba  

Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila kiumbe kitambaacho nchini.


Hao ndio wana wa Hamu, kufuata jamaa zao, kwa lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.


Hizo ndizo jamaa za wana wa Nuhu, kufuata vizazi vyao, katika mataifa yao; na kwa hao mataifa yaligawanyika katika nchi baada ya gharika.


Kwa hao nchi za pwani za mataifa ziligawanyikana kuwa nchi zao, kila moja kwa lugha yake, kwa jamaa zao, kufuata mataifa yao.


BWANA akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.


BWANA Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;


Wala hawakujua ya kwamba Yusufu anawasikia, kwa sababu alizungumza nao kupitia kwa mkalimani.


Huondoa usemi wa hao walioaminiwa, Na kuondoa fahamu za wazee.


Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.


BWANA huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huitangua mipango ya watu.


Ee Bwana, uwaangamize, uzivuruge ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.


BWANA akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, BWANA?


Hutawaona watu wale wakali; watu wa maneno magumu usiyoweza kuyafahamu; wenye lugha ya kigeni usiyoweza kuielewa.


Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.


Angalia, nitaleta taifa juu yenu litokalo mbali sana, Ee nyumba ya Israeli, asema BWANA; ni taifa hodari, ni taifa la zamani sana, taifa ambalo hujui lugha yake, wala huyafahamu wasemayo.


Haya! Ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa wameingia watu wajinga au wasioamini, je! Hawatasema ya kwamba mna wazimu?


BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;