Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mika 5:9 - Swahili Revised Union Version

Mkono wako na uinuliwe juu ya adui zako, na adui zako wote wakauliwe mbali.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waisraeli watawashinda adui zao na kuwaangamiza kabisa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waisraeli watawashinda adui zao na kuwaangamiza kabisa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu asema, “Wakati huo nitawaondoa farasi wenu, na kuyaharibu magari yenu ya farasi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako, nao adui zako wote wataangamizwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako, nao adui zako wote wataangamizwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mkono wako na uinuliwe juu ya adui zako, na adui zako wote wakauawe mbali.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mika 5:9
15 Marejeleo ya Msalaba  

Inuka, Ee Mungu BWANA, uuinue mkono wako, Ee Mungu Usiwasahau wanyonge.


Ndipo alipowainulia mkono wake na kuwaapia, Ya kuwa atawaangamiza jangwani,


Mkono wako utawapata adui zako wote, Mkono wako wa kulia utawapata wanaokuchukia.


nami nitakuelekezea wewe mkono wangu, na kukutakasa takataka zako kabisa, na kukuondolea bati lako lote;


Nao watashuka, watalirukia bega la Wafilisti upande wa magharibi; nao pamoja watawateka wana wa mashariki; watanyosha mkono juu ya Edomu na Moabu; na wana wa Amoni watawatii.


BWANA, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako.


Basi, sasa nitasimama; asema BWANA; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza.


Basi malaika wa BWANA alitoka, akaua watu elfu mia moja na themanini na tano katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.


nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake.


Na gari la vita nitaliondoa liwe mbali na Efraimu, na farasi awe mbali na Yerusalemu, na upinde wa vita utaondolewa mbali; naye atawahubiria mataifa yote habari za amani; na mamlaka yake yatakuwa toka bahari hata bahari, na toka Mto hata miisho ya dunia.


Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa muwachinje mbele yangu.


Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke adui zake wote chini ya miguu yake.