Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 31:5 - Swahili Revised Union Version

Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wakinywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wakinywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wakinywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote waliodhulumiwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 31:5
9 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa, Ben-hadadi alipolisikia neno hilo, naye alikuwa akinywa, yeye na wafalme, mabandani, aliwaambia watumwa wake, Jipangeni. Wakajipanga juu ya mji.


Usipotoe hukumu ya mtu maskini katika neno lake.


Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki; naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki; Hao wote wawili ni chukizo kwa BWANA.


Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.


Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, na walio hodari wa kuchanganya vileo;


wampao haki mwenye uovu, ili wapewe ijara, na kumwondolea mwenye haki haki yake!


Usinywe divai wala kileo chochote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;


Naam, pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu chungu.


Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.