Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 3:10 - Swahili Revised Union Version

Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na vyombo vyako vitafurika divai mpya.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hapo ghala zako zitajaa nafaka, na mapipa yako yatafurika divai mpya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hapo ghala zako zitajaa nafaka, na mapipa yako yatafurika divai mpya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hapo ghala zako zitajaa nafaka, na mapipa yako yatafurika divai mpya.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na vyombo vyako vitafurika divai mpya.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 3:10
15 Marejeleo ya Msalaba  

Azaria kuhani mkuu, wa nyumba ya Sadoki, akamjibu, akasema, Tangu watu walipoanza kuleta matoleo nyumbani kwa BWANA, tumekula na kushiba, na kusaza tele; kwa kuwa BWANA amewabariki watu wake; na kilichosalia ndiyo akiba hii kubwa.


Na katika kila kazi aliyoanza kwa utumishi wa nyumba ya Mungu, na kwa torati, na kwa amri, ili kumtafuta Mungu wake, aliifanya kwa moyo wake wote, akafanikiwa.


Ghala zetu na zijae Zenye akiba za jinsi zote. Kondoo zetu na wazae Elfu na makumi elfu mashambani mwetu.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.


Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta.


Je, Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki.


Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa angaa kikombe cha maji baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake.


na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba BWANA, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.


BWANA ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako.