Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:8 - Swahili Revised Union Version

Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wenye dharau huutia vurugu mji mzima, lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wenye dharau huutia vurugu mji mzima, lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wenye dharau huutia vurugu mji mzima, lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wanaodhihaki huuchochea mji, bali wenye hekima huzuia hasira.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:8
19 Marejeleo ya Msalaba  

Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki; Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.


Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.


Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.


Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.


Ndipo BWANA akaniambia, Hata wangesimama mbele zangu Musa na Samweli, moyo wangu usingewaelekea watu hawa; watupe, watoke mbele za macho yangu, wakaende zao.


Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.


Akasimama kati ya hao waliokufa na hao waliokuwa wangali hai; tauni ikazuiwa.


Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, amezigeuza hasira zangu zisiwe juu ya wana Wa Israeli, kwa kuwa alikuwa na wivu kati yao kwa wivu wangu mimi, hata nisiwaangamize wana wa Israeli katika wivu wangu.