Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 16:14 - Swahili Revised Union Version

14 Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo; mtu mwenye busara ataituliza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo; mtu mwenye busara ataituliza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo; mtu mwenye busara ataituliza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti, bali mtu mwenye hekima ataituliza.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti, bali mtu mwenye hekima ataituliza.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

14 Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.

Tazama sura Nakili




Methali 16:14
18 Marejeleo ya Msalaba  

Farao akawaghadhibikia maofisa wake wawili, mkuu wa wanyweshaji na mkuu wa waokaji.


Mfalme akaondoka kwa ghadhabu kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.


Midomo ya haki ni furaha ya wafalme; Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.


Kuna uhai katika nuru ya uso wa mfalme, Na fadhili zake ni kama wingu la masika.


Mtu mwovu hataki neno ila kuasi tu; Kwa hiyo mjumbe mkali atatumwa kwake.


Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; Bali hisani yake kama umande juu ya majani.


Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.


Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa BWANA


Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.


Roho yake mtawala ikiinuka kinyume chako, Usiondoke mara mahali pako ulipo; Kwa maana roho ya upole hutuliza machukizo yaliyo makubwa.


Basi Danieli akaingia, akamwomba mfalme ampe muda, kisha yeye atamwonesha mfalme tafsiri ile.


Mara mfalme akatuma askari, akaamuru kuleta kichwa chake. Basi akaenda, akamkata kichwa mle gerezani,


Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulala, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme.


Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo