Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 26:2 - Swahili Revised Union Version

Kama shomoro katika kutangatanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpati mtu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua, kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua, kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua, kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kama shomoro katika kutangatanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpati mtu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 26:2
10 Marejeleo ya Msalaba  

Labda BWANA atayaangalia mabaya yaliyonipata, naye BWANA atanilipa mema kwa sababu ya kunilaani kwake leo.


BWANA amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya Sauli ambaye umetawala badala yake; naye BWANA ametia ufalme katika mkono wa Absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu.


kwa sababu hawakuwalaki wana wa Israeli kwa chakula na maji, bali walimwajiri Balaamu juu yao ili awalaani; lakini Mungu aliigeuza ile laana kuwa baraka.


Waache walaani, bali Wewe utabariki, Wanaonishambulia na waaibishwe, Naye mtumishi wako afurahi.


Kama ndege aendaye huku na huko mbali na kitundu chake; Ndivyo alivyo mtu aendaye huku na huko mbali na mahali pake.


Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huku na huko, kama kiota cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni.


Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani? Nimshutumuje, yeye ambaye BWANA hakumshutumu?


Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.