Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 14:5 - Swahili Revised Union Version

Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Shahidi mwaminifu hasemi uongo, lakini asiyeaminika hububujika uongo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Shahidi mwaminifu hasemi uongo, lakini asiyeaminika hububujika uongo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Shahidi mwaminifu hasemi uongo, lakini asiyeaminika hububujika uongo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Shahidi mwaminifu hadanganyi, bali shahidi wa uongo humimina uongo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Shahidi mwaminifu hadanganyi, bali shahidi wa uongo humimina uongo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 14:5
15 Marejeleo ya Msalaba  

Na hao watu wawili, watu wasiofaa, wakaingia, wakaketi mbele yake; wale watu wasiofaa wakamshuhudia Nabothi mbele ya watu, wakasema, Nabothi amemtukana Mungu na mfalme. Ndipo wakamchukua nje ya mji, wakampiga kwa mawe hata akafa.


Usimshuhudie jirani yako uongo.


Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.


Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.


Mwenye haki huchukia kusema uongo; Bali mtu mbaya huwa karaha, hupatwa na aibu.


Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu; Bali atoaye uongo hudanganya.


Zizi ni safi ambapo hapana ng'ombe; Bali nguvu za ng'ombe zaleta faida nyingi.


Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate; Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.


Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.


Shahidi mdhalimu akimwinukia mtu yeyote na kushuhudia juu yake ya upotoe;


tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,


Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.