Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 12:20 - Swahili Revised Union Version

Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni, lakini wanaonuia mema hupata furaha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni, lakini wanaonuia mema hupata furaha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni, lakini wanaonuia mema hupata furaha.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 12:20
16 Marejeleo ya Msalaba  

Akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA kama nyumba ya Ahabu; kwa kuwa hao walikuwa washauri wake, baada ya kifo cha baba yake, hata aangamie.


Umewakataa wote wazikosao amri zako, Kwa maana hila zao ni bure.


Asiye haki hutamani nyavu za wabaya; Bali shina lao wenye haki huleta matunda.


Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.


Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote; Bali wasio haki watajazwa mabaya.


Mimi hapa sikufanya haraka kuacha kuwa mchungaji nyuma yako; wala sikuitamani siku ya maradhi ya kuua; wewe unajua; yaliyotoka midomoni mwangu yalikuwa mbele za uso wako.


Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa.


Naam, yeye atalijenga hekalu la BWANA; naye atakuwa na heshima ya kifalme; na ataketi na kutawala; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na maelewano yenye amani yatakuwa kati ya hao wawili.


Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.


Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,


Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;