Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 23:12 - Swahili Revised Union Version

Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 23:12
15 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.


Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Basi mimi, Nebukadneza, namhimidi Mfalme wa mbinguni, namtukuza na kumheshimu; maana matendo yake yote ni kweli, na njia zake ni za adili; na wale waendao kwa kutakabari, yeye aweza kuwadhili.


Basi, yeyote ajinyenyekezaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.


Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;