Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 9:8 - Swahili Revised Union Version

Musa akawaambia, Ngojeni hapo; hata nipate sikiza BWANA atakaloagiza juu yenu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka hapo nitakapopata maagizo juu yenu kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka hapo nitakapopata maagizo juu yenu kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka hapo nitakapopata maagizo juu yenu kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Musa akawajibu, “Ngojeni hadi nitafute kile Mwenyezi Mungu anachoagiza kuwahusu ninyi.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Musa akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Musa akawaambia, Ngojeni hapo; hata nipate kumsikiliza BWANA atakaloniagiza juu yenu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 9:8
19 Marejeleo ya Msalaba  

Hamtahitaji kupigana vita, jipangeni, simameni, mkauone wokovu wa BWANA ulio pamoja nanyi, enyi Yuda na Yerusalemu; msiogope, wala msifadhaike; kesho tokeni juu yao; kwa kuwa BWANA yuko pamoja nanyi.


Siri ya BWANA iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.


Na nisikie atakavyosema Mungu BWANA, Maana atawaambia watu wake amani, Naam, na watauwa wake pia, Bali wasiurudie upumbavu tena.


Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.


Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu;


Nawe utawaambia maneno yangu, iwe watasikia au hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.


Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.


Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno litakalotoka kinywani pa BWANA.


Nao wakamweka kifungoni, maana, lilikuwa halijasemwa atakalotendwa.


Basi Musa akaleta neno lao mbele ya BWANA


Sisi tuko katika hali ya unajisi kwa ajili ya maiti wa mtu; nasi tumezuiwa kwa nini hata tusipate kumtolea BWANA matoleo kwa wakati wake ulioagizwa, kati ya wana wa Israeli?


BWANA akanena na Musa, akamwambia,


Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nilitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.


Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.


Kwa maana mimi nilipokea kwa Bwana niliyowapa nanyi, ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,


Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.