Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Yohana 2:3 - Swahili Revised Union Version

Na katika hili tunajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na katika hili tunajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Yohana 2:3
26 Marejeleo ya Msalaba  

Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, Utakaponipanulia ufahamu wangu.


Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.


Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.


Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, lakini hamyatendi nisemayo?


Mkinipenda, mtazishika amri zangu.


Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.


Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.


Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.


Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.


naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;


Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba.


Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana tunawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti.


Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake,


Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua.


Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake.


Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.


Tunajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu.


Katika hili tunajua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake.


Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.


Joka likamkasirikia yule mwanamke, likaenda zake lifanye vita juu ya wazawa wake waliobakia, wanaozishika amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; nalo likasimama juu ya mchanga wa bahari.


Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.


Heri wazifuao nguo zao, ili wawe na haki ya kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.