Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Yohana 5:3 - Swahili Revised Union Version

3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Huku ndiko kumpenda Mungu, yaani kuzitii amri zake. Nazo amri zake si nzito.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Huku ndiko kumpenda Mungu, yaani, kuzitii amri zake. Nazo amri zake si nzito.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

Tazama sura Nakili




1 Yohana 5:3
26 Marejeleo ya Msalaba  

Maana alishikamana na BWANA, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake BWANA alizomwamuru Musa.


Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.


Nami nitakwenda kwa uhuru, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.


nami nawarehemu maelfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.


Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.


Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake;


Ee mwanadamu, yeye amekuonesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!


Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.


Mkinipenda, mtazishika amri zangu.


Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.


Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.


Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.


Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani,


nami nawarehemu maelfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.


Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hadi vizazi elfu;


Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika fikira zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.


Na katika hili tunajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake.


Na huu ndio upendo: tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende kwayo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo