Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Samueli 30:4 - Swahili Revised Union Version

Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakapaza sauti zao na kulia, hadi walipokuwa hawana nguvu za kulia tena.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ndipo Daudi na watu wake walipoangua kilio, wakalia hadi walipoishiwa nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ndipo Daudi na watu wake walipoangua kilio, wakalia hadi walipoishiwa nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ndipo Daudi na watu wake walipoangua kilio, wakalia hadi walipoishiwa nguvu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hivyo Daudi na watu wake wakapaza sauti na kulia hadi wakaishiwa na nguvu za kulia.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakapaza sauti zao na kulia, hadi walipokuwa hawana nguvu za kulia tena.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Samueli 30:4
9 Marejeleo ya Msalaba  

Basi hapo Ezra alipokuwa akiomba na kuungama, akilia, na kujiangusha kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu, kusanyiko kubwa sana la wanaume, wanawake na watoto, kutoka katika Israeli likamkusanyikia; maana watu hao walikuwa wakilia sana.


Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule.


Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli wote maneno haya, na hao watu wakaomboleza sana.


Ikawa, hapo huyo malaika wa BWANA alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia.


Basi hao watu wakafika Betheli, wakaketi huko mbele ya Mungu hadi jioni, nao wakainua sauti zao na kulia sana.


Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia.


Basi Daudi na watu wake walipoufikia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, wanaume kwa wanawake, wamechukuliwa mateka.


Alipofika, tazama, Eli alikuwa ameketi kitini pake kando ya njia, akingojea; maana moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Na yule mtu alipoingia mjini, akatoa habari, mji wote ukalia.