Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 26:1 - Swahili Revised Union Version

Ee BWANA, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini BWANA bila wasiwasi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ee Mwenyezi-Mungu, unitetee, maana nimeishi bila hatia, nimekutumainia wewe bila kusita.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ee Mwenyezi-Mungu, unitetee, maana nimeishi bila hatia, nimekutumainia wewe bila kusita.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ee Mwenyezi-Mungu, unitetee, maana nimeishi bila hatia, nimekutumainia wewe bila kusita.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Mwenyezi Mungu, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Mwenyezi Mungu bila kusitasita.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia bwana bila kusitasita.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee BWANA, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini BWANA bila wasiwasi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 26:1
30 Marejeleo ya Msalaba  

Nakusihi, BWANA, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.


BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ijapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.


Je! Dini yako siyo tegemeo lako? Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?


Hatauacha mguu wako usogezwe; Akulindaye hatasinzia;


Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,


Kwa kuwa mfalme humtumainia BWANA, Na kwa fadhili zake Aliye Juu hatatikisika.


Ee Mungu wangu, Nimekutumainia Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.


Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.


Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.


BWANA ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru.


Lakini mimi nakutumaini Wewe, BWANA, Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.


Unihukumu kwa haki yako, Ee BWANA, Mungu wangu, Na usiwaache wanisimange.


Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake. Hatua zake hazitelezi.


Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini BWANA.


Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.


Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe, Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.


Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.


Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.


BWANA atawaamua mataifa, BWANA, unihukumu mimi, Kwa kadiri ya haki yangu, Kulingana na unyofu nilio nao.


Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee BWANA, fadhili zako zilinitegemeza.


Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.


Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.


Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.


Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu;


Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani ili mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.


Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.


Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake; Bali waovu watanyamazishwa gizani, Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;


Basi BWANA atuamue, akatuhukumu mimi na wewe, akaone, akanitetee neno langu, akaniokoe kutokana na mkono wako.