Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yoeli 1:8 - Swahili Revised Union Version

Omboleza kama mwanamwali avaaye magunia Kwa ajili ya mume wa ujana wake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lieni kama msichana aliyevaa vazi la gunia akiombolezea kifo cha mchumba wake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lieni kama msichana aliyevaa vazi la gunia akiombolezea kifo cha mchumba wake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lieni kama msichana aliyevaa vazi la gunia akiombolezea kifo cha mchumba wake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Omboleza kama bikira aliyevaa gunia akimwomboleza mume wa ujana wake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Omboleza kama bikira aliyevaa nguo ya gunia anayehuzunika kwa ajili ya mume wa ujana wake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Omboleza kama mwanamwali avaaye magunia Kwa ajili ya mume wa ujana wake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yoeli 1:8
13 Marejeleo ya Msalaba  

Amwachaye rafiki wa ujana wake, Na kulisahau agano la Mungu wake.


Siku hiyo Bwana, BWANA wa majeshi, akawaita watu walie na kuomboleza, na kung'oa nywele zao, na kuvaa nguo za magunia;


Tetemekeni, enyi wanawake mnaostarehe; taabikeni, enyi msiokuwa na uangalifu; jivueni, jivueni nguo zenu kabisa, na kujivika nguo za magunia viunoni.


Je, tokea wakati huu hutanililia, Ee Baba yangu, wewe u kiongozi wa ujana wangu?


Njia za Sayuni zaomboleza, Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu; Malango yake yote yamekuwa ukiwa, Makuhani wake hupiga kite; Wanawali wake wanahuzunika; Na yeye mwenyewe huona uchungu.


Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upara katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.


Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzawa mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana.


Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige mayowe kwa sababu ya mateso yenu yanayowajia.