Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yoeli 1:7 - Swahili Revised Union Version

7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Limeiharibu mizabibu yetu, na kuitafuna mitini yetu. Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini, na matawi yake yameachwa meupe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Limeiharibu mizabibu yetu, na kuitafuna mitini yetu. Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini, na matawi yake yameachwa meupe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Limeiharibu mizabibu yetu, na kuitafuna mitini yetu. Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini, na matawi yake yameachwa meupe.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Limeharibu mizabibu yangu na kuangamiza mitini yangu. Limebambua magome yake na kuyatupilia mbali, likayaacha matawi yake yakiwa meupe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Limeharibu mizabibu yangu na kuangamiza mitini yangu. Limebambua magome yake na kuyatupilia mbali, likayaacha matawi yake yakiwa meupe.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.

Tazama sura Nakili




Yoeli 1:7
12 Marejeleo ya Msalaba  

Akaipiga mizabibu yao na mitini yao, Akaivunja miti ya nchi yao.


Na hao nzige wakakwea juu ya nchi yote ya Misri, wakatua ndani ya mipaka yote ya Misri, walikuwa wabaya mno; hawajakuwapo nzige kama hao majira yoyote, wala baada yao hawatakuwa wengine jinsi hiyo.


Kwa kuwa waliufunika uso wote wa nchi, hata nchi iliingia giza; wakala mimea yote ya nchi, na matunda yote ya miti yaliyosazwa na ile mvua ya mawe; hapakusalia hata jani moja, mti wala mmea wa mashamba, katika nchi yote ya Misri.


Divai mpya inaomboleza, mzabibu umedhoofika, watu wote waliochangamka moyo wanaugua.


Watajipiga vifua kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mzabibu uliozaa sana.


nami nitaliharibu; wala halitapogolewa wala kulimwa, bali litamea mbigili na miiba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Nitawaangamiza kabisa, asema BWANA; hapana zabibu katika mizabibu, wala tini katika mitini, hata jani lake litanyauka; na vitu vile nilivyowapa vitawapotea.


Nami nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema, Hii ndiyo ujira wangu niliopewa na wapenzi wangu; nami nitaifanya kuwa msitu, na wanyama wa mashamba wataila.


Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imetoweka kwa wanadamu.


Nami nimewapiga kwa ukame na kuvu; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema BWANA.


Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula; Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe;


Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo