Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yakobo 1:15 - Swahili Revised Union Version

Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi ile tamaa mbaya ikishachukua mimba huzaa dhambi, nayo ile dhambi ikikomaa huzaa mauti.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi ile tamaa mbaya ikishachukua mimba, huzaa dhambi, nayo ile dhambi ikikomaa, huzaa mauti.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yakobo 1:15
21 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”


Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alichuma matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.


Basi Daudi akatuma wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.


Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Na mioyo yao hutunga udanganyifu.


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Wadhalimu wataenda kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.


Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.


Ninyi mtachukua mimba ya makapi, mtazaa majani makavu; pumzi yenu ni moto utakaowateketeza wenyewe.


Hakuna anayeshitaki kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.


Wakati huo mmoja wa wale Kumi na Wawili, jina lake Yuda Iskarioti, aliwaendea wakuu wa makuhani,


lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.


Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.


Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.