Nehemia 5:13 - Swahili Revised Union Version
Tena nikakung'uta nguo yangu, nikasema, Mungu na amkung'ute vivyo hivyo kila mtu nyumbani mwake, na kazini mwake, asiyeitimiza ahadi hiyo; naam, na akung'utwe vivyo hivyo, na kuwa hana kitu. Mkutano wote wakasema, Amina; wakamhimidi BWANA. Nao watu wakafanya kama walivyoahidi.
Tazama sura
Matoleo zaidi
Nilikunguta kibindo changu na kusema, “Kila mmoja asiyetimiza ahadi hii Mungu na amkungute, amtoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akungutike na kubaki mikono mitupu.” Mkutano mzima ukaitikia, na kusema, “Amina” wakamsifu Mwenyezi-Mungu. Watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Tazama sura
Nilikunguta kibindo changu na kusema, “Kila mmoja asiyetimiza ahadi hii Mungu na amkungute, amtoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akungutike na kubaki mikono mitupu.” Mkutano mzima ukaitikia, na kusema, “Amina” wakamsifu Mwenyezi-Mungu. Watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Tazama sura
Nilikung'uta kibindo changu na kusema, “Kila mmoja asiyetimiza ahadi hii Mungu na amkung'ute, amtoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akung'utike na kubaki mikono mitupu.” Mkutano mzima ukaitikia, na kusema, “Amina;” wakamsifu Mwenyezi-Mungu. Watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Tazama sura
Pia nikakung’uta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkung’ute hivi kutoka nyumba yake na katika mali yake. Basi mtu kama huyo akung’utiwe nje na aachwe bila kitu!” Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza Mwenyezi Mungu. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Tazama sura
Pia nikakung’uta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkung’ute hivi kutoka nyumba yake na katika mali zake. Basi mtu wa namna hiyo akung’utiwe nje na aachwe bila kitu!” Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza bwana. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Tazama sura
Tena nikakung'uta nguo yangu, nikasema, Mungu na amkung'ute vivyo hivyo kila mtu nyumbani mwake, na kazini mwake, asiyeitimiza ahadi hiyo; naam, na akung'utwe vivyo hivyo, na kuwa hana kitu. Mkutano wote wakasema, Amina; wakamhimidi BWANA. Nao watu wakafanya kama walivyoahidi.
Tazama sura
Tafsiri zingine