Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 18:15 - Swahili Revised Union Version

Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo! Umecheka.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Sara akaogopa, hivyo akadanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Mwenyezi Mungu akasema, “Ndiyo, ulicheka!”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Sara akakana, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo! Umecheka.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 18:15
17 Marejeleo ya Msalaba  

Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako.


Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.


Kisha watu hao wakaondoka huko wakaelekeza nyuso zao Sodoma. Abrahamu akaenda pamoja nao awasindikize.


BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, kwani mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?


Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.


Je! Mungu hangegundua jambo hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.


Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kama kondoo waendao kuchinjwa.


Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.


Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.


Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?


Basi yule kijakazi, aliyekuwa mlinda mlango, akamwambia Petro, Wewe nawe, je! Hu mwanafunzi mmojawapo wa mtu huyu? Naye akasema, Si mimi.


na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.


Basi twajua ya kuwa mambo yote inenayo torati huyanena kwa hao walio chini ya torati, ili kila kinywa kifumbwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu;


na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;


Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;


Tukisema kwamba hatuna dhambi, tunajidanganya wenyewe, wala kweli haimo ndani yetu.