Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mwanzo 18:15 - Swahili Revised Union Version

15 Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo! Umecheka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Lakini Sara, akiwa na hofu, akakana akisema, “Sikucheka!” Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Sivyo! Kucheka, ulicheka.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Sara akaogopa, hivyo akadanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Mwenyezi Mungu akasema, “Ndiyo, ulicheka!”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

15 Sara akakana, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo! Umecheka.

Tazama sura Nakili




Mwanzo 18:15
17 Marejeleo ya Msalaba  

Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako.


Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.


Kisha watu hao wakaondoka huko wakaelekeza nyuso zao Sodoma. Abrahamu akaenda pamoja nao awasindikize.


BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, kwani mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?


Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.


Je! Mungu hangegundua jambo hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.


Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kama kondoo waendao kuchinjwa.


Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.


Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.


Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?


Basi yule kijakazi, aliyekuwa mlinda mlango, akamwambia Petro, Wewe nawe, je! Hu mwanafunzi mmojawapo wa mtu huyu? Naye akasema, Si mimi.


na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.


Basi twajua ya kuwa mambo yote inenayo torati huyanena kwa hao walio chini ya torati, ili kila kinywa kifumbwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu;


na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;


Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;


Tukisema kwamba hatuna dhambi, tunajidanganya wenyewe, wala kweli haimo ndani yetu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo