Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 28:5 - Swahili Revised Union Version

Watu waovu hawaelewi na haki; Bali wamtafutao BWANA huelewa na zote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waovu hawajui maana ya haki, lakini wamchao Mwenyezi-Mungu wanaielewa kabisa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waovu hawajui maana ya haki, lakini wamchao Mwenyezi-Mungu wanaielewa kabisa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waovu hawajui maana ya haki, lakini wamchao Mwenyezi-Mungu wanaielewa kabisa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wapotovu hawaelewi haki, bali wale wanaomtafuta Mwenyezi Mungu wanaielewa kikamilifu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao bwana wanaielewa kikamilifu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Watu waovu hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao BWANA huelewa na yote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 28:5
18 Marejeleo ya Msalaba  

Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.


Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote.


Siri ya BWANA iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.


Mtu mjinga hayatambui hayo, Wala mpumbavu hayafahamu.


Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.


Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, Na adili, na kila njia njema.


Kwa mpumbavu hekima haipatikani; Hafumbui kinywa chake langoni.


Ng'ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.


Hawajui wala hawafikiri; maana amewafumba macho, wasione, na mioyo yao, wasiweze kufahamu.


Naye akaniambia, Nenda, ukawaambie watu hawa, Endeleeni kusikia, lakini msifahamu; endeleeni kutazama, lakini msione.


Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.


Kwa maana hawajui kutenda haki, asema BWANA, hao wawekao akiba ya jeuri na unyang'anyi katika majumba yao.


Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.


Lakini mmoja wenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.


Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote.


Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.