Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 23:7 - Swahili Revised Union Version

Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

maana moyoni mwake anahesabu unachokula. Atakuambia, “Kula, kunywa!” Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

maana moyoni mwake anahesabu unachokula. Atakuambia, “Kula, kunywa!” Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

maana moyoni mwake anahesabu unachokula. Atakuambia, “Kula, kunywa!” lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri kuhusu gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 23:7
12 Marejeleo ya Msalaba  

Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;


Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Lakini yanakata kama upanga mkali.


Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.


Midomo ijipendekezayo pamoja na moyo mbaya Ni kama kigae kilichofunikizwa taka za fedha.


Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.


Anenapo maneno mazuri usimsadiki; Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.


Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa.


Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.


Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.