Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 26:24 - Swahili Revised Union Version

24 Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

24 Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri, lakini huwa ana hila moyoni mwake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

24 Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri, lakini huwa ana hila moyoni mwake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

24 Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri, lakini huwa ana hila moyoni mwake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

24 Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.

Tazama sura Nakili




Methali 26:24
17 Marejeleo ya Msalaba  

Wana wa Yakobo wakawajibu Shekemu na Hamori babaye, kwa hila, maana amemharibu Dina, dada yao,


Ndipo akasema Absalomu, Kama huji, nakusihi, mwache ndugu yangu Amnoni aende nasi.


Mfalme akamwambia, Kwa nini aende nawe? Lakini Absalomu akamsihi sana, naye akamwacha Amnoni na wana wote wa mfalme waende naye.


Naye Yoabu akamwambia Amasa, Amani kwako, ndugu yangu. Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kulia ili ambusu.


Sanbalati na Geshemu wakatuma wajumbe kwangu, wakasema, Njoo, tukutane huko vijijini katika nchi tambarare ya Ono. Lakini wakakusudia kunifanyia mabaya.


BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza, Na ulimi unenao maneno ya kiburi;


Usinikokote pamoja na wasio haki, Wala pamoja na watenda maovu. Wawaambiao jirani zao maneno ya amani, Lakini mioyoni mwao mna madhara.


Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, Moyo wake hujikusanyia maovu, Naye atokapo nje huyanena.


Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.


Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa BWANA; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.


Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.


Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.


Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.


Akili za mwenye busara ni kujua njia yake; Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.


Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.


Jihadharini, kila mtu na jirani yake, wala msimtumaini ndugu awaye yote; maana kila ndugu atachongea, na kila jirani atakwenda huku na huko na kusingizia.


Kisha Sauli akamwambia Daudi, Tazama, binti yangu mkubwa, Merabu, huyu nitakupa wewe ili umwoe; ila na wewe uniwie hodari wa vita, na kuvipiga vita vya BWANA. Maana Sauli alisema moyoni mwake, Mkono wangu usiwe juu yake, bali mkono wa Wafilisti na uwe juu yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo