Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 12:2 - Swahili Revised Union Version

2 Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Kila mmoja humdanganya mwenzake, husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Kila mmoja humdanganya mwenzake, husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Kila mmoja humdanganya mwenzake, husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;

Tazama sura Nakili




Zaburi 12:2
25 Marejeleo ya Msalaba  

Wa Zabuloni, watu wawezao kwenda pamoja na jeshi, hodari wa kupanga vita, wenye zana za vita za kila namna, elfu hamsini; askari stadi waliolenga tu kumsaidia Daudi.


Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,


Nikiwa katika hangaiko langu nikasema, Wanadamu wote ni waongo.


Uniponye, unitoe, Katika mkono wa wageni. Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa kulia ni mkono wa uongo.


Vinywa vyao vinasema visivyofaa, Na ambao mikono yao ya kulia ni ya uongo.


Usinikokote pamoja na wasio haki, Wala pamoja na watenda maovu. Wawaambiao jirani zao maneno ya amani, Lakini mioyoni mwao mna madhara.


Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.


Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, Moyo wake hujikusanyia maovu, Naye atokapo nje huyanena.


Maana vinywani mwao hamna uaminifu; Moyo wao ni shimo tupu, koo lao ni kaburi wazi, Ulimi wao hujipendekeza.


Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Lakini yanakata kama upanga mkali.


Kwa dhambi ya kinywa chao, Na kwa neno la midomo yao, Wanaswe kwa kiburi chao, Kwa ajili ya kulaani na uongo wasemao.


Mpango wao ni kumwangusha tu mtu mwenye cheo; Huufurahia uongo. Kwa kinywa chao hubariki; Kwa moyo wao hulaani.


Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.


Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?


Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.


Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya BWANA, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali na vinywa vyao.


Ulimi wao ni mshale ufishao; husema maneno ya hadaa; mtu mmoja husema maneno ya amani na mwenzake kwa kinywa chake, lakini moyoni mwake humwotea.


Kwa maana hayatakuwapo tena maono yoyote ya ubatili, wala ubashiri wa kujipendekeza, katika nyumba ya Israeli.


Mtu amchaye Mungu ametoweka, asionekane katika nchi, wala hapana mtu mwenye adili katika wanadamu; wote huotea ili kumwaga damu; kila mtu humwinda ndugu yake kwa wavu.


Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe; na kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu.


Maana hatukuwa na maneno ya kujipendekeza wakati wowote, kama mjuavyo, wala maneno ya juu juu ya kuficha choyo; Mungu ni shahidi.


Mtu wa nia mbili husitasita katika njia zake zote.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo