Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 15:1 - Swahili Revised Union Version

Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kujibu kwa upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kujibu kwa upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kujibu kwa upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 15:1
16 Marejeleo ya Msalaba  

Hao watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda, wakasema, Sisi tunazo sehemu kumi katika mfalme, tena tunayo haki yetu katika Daudi zaidi kuliko ninyi; mbona basi ninyi mmetudharau sisi, msitake ushauri wetu kwanza katika kumrudisha tena mfalme wetu? Na maneno ya watu wa Yuda yakawa makali kuliko maneno ya watu wa Israeli.


Wakamwambia wakasema, Ukikubali kuwa mtumishi wa watu hawa leo, na kuwatumikia, na kuwajibu, na kuwapa maneno mazuri, basi watakuwa watumishi wako daima.


Wakamwambia, wakasema, Ukiwa mwema kwao watu hawa, na kuwapendeza, na kuwaambia maneno mazuri, hapo watakuwa watumishi wako siku zote.


Je! Atakusihi sana? Au, atakuambia maneno ya upole?


Kuchukiana huleta fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.


Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa.


Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina; Bali amtumainiye BWANA ataneemeshwa.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.


Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.


Alipokwisha kusema haya akauvunja mkutano.