Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 1:9 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

hayo yatakupamba kilemba kichwani pako, kama mkufu shingoni mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

hayo yatakupamba kilemba kichwani pako, kama mkufu shingoni mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

hayo yatakupamba kilemba kichwani pako, kama mkufu shingoni mwako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 1:9
16 Marejeleo ya Msalaba  

Farao akavua pete yake ya mhuri mkononi mwake, akaitia mkononi mwa Yusufu; akamvika mavazi ya kitani nzuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake.


Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Udhalimu huwavika kama nguo.


Basi yatakuwa uzima kwa nafsi yako, Na neema shingoni mwako.


Rehema na kweli zisiachane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.


Atakupa neema kuwa kilemba kichwani; Na kukukirimia taji la uzuri.


Mashavu yako ni mazuri kwa mashada, Shingo yako kwa mikufu ya vito.


Umenishangaza moyo, dada yangu, Bibi arusi, umenishangaza moyo, Kwa mtupo mmoja wa macho yako, Kwa mkufu mmoja wa shingo yako.


na pete za masikio, na vikuku, na mataji yao;


Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;


Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.


Lakini nimesikia habari zako, kwamba waweza kuleta tafsiri, na kufumbua mafumbo; haya! Kama ukiweza kulisoma andiko hili, na kunijulisha tafsiri yake, utavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utakuwa mtu wa tatu katika ufalme.


Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake, wakapiga mbiu kutangaza habari zake, ya kwamba yeye ni mtu wa tatu katika ufalme.


Mfalme akalia kwa sauti kubwa, akaamuru waletwe wachawi, na Wakaldayo na wanajimu. Mfalme akanena, akawaambia wenye hekima wa Babeli, mtu awaye yote atakayesoma maandiko haya, na kunionesha tafsiri yake, atavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atakuwa mtu wa tatu katika ufalme.